Wajumbe mbalimbali kwenye bunge la
katiba wameendelea kuwasha vipaza sauti vyao kuchangia, kutoa ya moyoni kwa
kujadili sura ya kwanza na ya sita huku ishu ya serikali mbili au tatu
ikizimiliki headlines zaidi.
Kauli za mjumbe Mh. Joseph Mbilinyi
ambae pia ni mbunge wa Mbeya Mjini alizozitoa trh. 15/April/2014.
‘Wabunge Wakristo hii ni kwaresma,
ni kipindi cha toba… mnatumia kipindi hiki kufanya unafiki mbele ya Wananchi
mtakuja kuhukumiwa siku itakapofika, wameharibu mchakato wakati tumeshatumia
mabilioni mengi ya hela’
‘Ukarabati tu wa jengo la bunge hili
ili sisi tukae zimetumika BILIONI 8.2 alafu leo kwa sababu ya hotuba moja tu ya
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wote wamegeuka, wanaharibu kabisa tunashindwa
kufanya mambo ya maana, wanaacha kupanga mkakati wa hoja wanapanga mkakati wa
kuzomea, wameishiwa mikakati mpaka wanazomea kimkakati’
‘Unakutana na mbunge tena Waziri
kama rafiki yangu Mwigulu Nchemba tunataniana ananiita mzee wa Maandamano mi
namuita mzee wa kuteka, ananiambia wewe Sugu sijui unataka serikali tatu sijui
vipi na vipi, namwambia kwani hutaki kabisa Tanganyika anasema mi nataka
Tanganyika ila nataka serikali moja, sasa kama mnataka serikali moja kwa nini
uibuke kwenye hoja ya serikali mbili?
‘Kuna watu ambao wanajadili vitu
ambavyo