Siku 4 zimepita tangu klabu ya
soka nchini inayoshiriki ligi kuu Tanzania bara, Azam FC kuingia katika orodha
ya klabu zilizotwaa ubingwa wa ligi kuu nchini kwa mara ya kwanza katika
historia yake. Lakini kumezuka hadithi miongoni mwa wadau wa soka sehemu
tofauti tofauti nchini zikiihusisha klabu ya Azam na ishu ya kuhonga wachezaji
na viongozi wa timu nyingine ili washinde game zao hatimaye kutwaa ubingwa
wako.
Kupitia Facebook, hii ni kauli ya Azam FC kufuatia
hadithi ya kuhonga wachezaji na viongozi wa timu nyingine ili washinde michezo
yao kuelekea tamati ya ligi kuu hata kutwaa ubingwa msimu huu >>
“Maneno yanayozungumzwa ni
porojo Baada ya Azam Fc kupata mafanikio ya
kuwa bingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Azam Fc ilipata nafasi ya pili mara
Mbili katika Ligi Kuu ya Tanzania bara haikuwai kusemwa imenunua leo iweje
imekuwa Bingwa isemwe imenunua.
John Bocco ameweka Historia Baada ya Kufunga Goli la Ushindi ktk Mechi
ya Mwisho ya Ligi Daraja la kwanza na Kuipandisha Azam Fc kucheza Ligi kuu ya
Tanzania Bara, na leo Hii Tumeshuhudia John Bocco ameweka Historia ya Kufunga
Goli la Ushindi na Kuipa Timu ya Azam Fc Ubingwa kwa Mara ya kwanza Tangu
ilipopanda Daraja kucheza ligi kuu ya Tanzania Bara kwa Msimu 2013/2014 na
kucheza Bila kupoteza hata mechi Moja.
Hatuto puuzia mechi ya mwisho Dhidi ya JKT Ruvu Tutacheza kama mechi
nyingine Tulivyocheza Tunahitaji kuweka Historia ya Kutokupoteza hata Mechi
Moja kwa Msimu Huu JKT Ruvu wajiandae kwa Kichapo wakati Tukiwa Tunakabidhiwa
Kombe letu la Msimu Huu
Baadhi ya Maneno ambayo Makocha wanazungumza Sio Mazuri wao kama
wataalam hawatakiwi kujihusisha katika Propaganda ambazo baadhi ya watu
wanaziendeleza.”
Na. Gwalugano ‘Godb’ Mwakalobo