Saturday, March 29, 2014

HUU NI MSIMAMO WA LIGI KUU UINGEREZA BAADA YA MICHEZO YOTE.........



MATOKEO:

Man United 4 - 1 Aston Villa
Stoke City 1 - 0 Hull City
Swansea City 3 - 0 Norwich City
Southampton 4 - 0 Newcastle United
West Bromwich Albion 3 - 3 Cardiff City
Crystal Palace 1 - 0 Chelsea
Arsenal 1 – 1 Manchester City


KIAFRIKA ZAIDI...SIKILIZA NA PAKUA Azonto ya Fuse ODG ft. Tiffany HAPA...

MAN UNITED YANUSURU KIBARUA CHA MOYES !



Hii leo Manchester United imeicharua mabao 4-1 Aston Villa katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza ambapo Manchester United walikuwa wenyeji wa mchezo huo katika uwanja wao wa Old Trafford.

Aston Villa alikuwa wa kwanza kupata bao la kwanza la kuongoza  kupitia nyota wake Westwood katika dakika ya 13 ya kipindi cha kwanza.

Manchester United ilijibu mashambulizi kwa kusawazisha bao la Aston Villa kupitia mshambuliaji wake Wayne Rooney dakika ya 20 na kuongeza bao jingine la kuongoza dakika ya 45 kipindi cha kwanza. Mabao mengine ya Manchester United yalifungwa na Juan Mata katika dakika ya 57 na Chicharito kufunga hesabu dakika ya 90.

Haya ni matokeo ya mchezo mingine ya leo ya ligi kuu ya Uingereza:

Stoke City 1 - 0 Hull City,
Swansea City 3 - 0 Norwich City,
Southampton 4 - 0 Newcastle United,
West Bromwich Albion 3 - 3 Cardiff City,
Crystal Palace 1 - 0 Chelsea na
Arsenal 1 – 1 Manchester City

Tuesday, March 25, 2014

UMOJA WA MATAIFA WALAANI HUKUMU YA VIFO MISRI

Umoja wa Mataifa umelaani kitendo cha Misri kuwahukumu kifo zaidi ya watu miatano ikisema kuwa ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa za haki za binadamu

Sunday, March 23, 2014

JE WAJUA.. ASALI NI CHAKULA PEKEE KISICHO.................?



Asali ndiyo chakula pekee duniani kisichoharibika katu.

Wanasayansi wamethibitisha hilo baada ya kupima asali iliyopatikana katika kaburi la Farao wa Misri na kukuta ni nzima mpaka sasa.

kama hukutazama mechi ya MAN UNITED dhidi ya WESTHAM UNITED... CHEKI HILI GOLI LA PILI LA ROONEY...

Inasemekana ni goli zuri kutokea katika msimu huu hususani mwezi huu... Lilikuwa ni bao la pili la kuongoza na la ushindi kwa Manchester United dhidi ya Westham United. Alifunga mwenyewe bao la kwanza pia katika ushindi wa bao 2-0.

MAUAJI TENA KENYA!



Lokoni, Mombasa

Watu wawili wameuawa na wengine 10 kujeruhiwa baada ya mtu mmoja kufyatua risasi ndani ya kanisa la Joy Jesus huko Lokoni, Mombasa.

Chanzo Global Publisher

TEMBEA UONE........