Friday, April 18, 2014

Ujumbe wa ZITTO KABWE KUELEKEA PASAKA


“Katiba ni mwafaka wa Taifa. Uandishi wa Katiba ni ujenzi wa mwafaka huo. Majadiliano ya Rasimu ya Katiba ni mchakato wa uandishi wa Katiba hiyo. Majadiliano ya upande mmoja yanaweza kuwa halali kisheria (legal legitimacy) lakini yanakosa uhalali wa kisiasa ( political legitimacy). Lazima kujenga mwafaka kwa kuhakikisha makundi yote yanashiriki katika kupata katiba ya wananchi. Asitokee wa kujidanganya kuwa kundi moja la nchi laweza kuandika katiba peke yake na ikakubaliwa na watu. Tutumie fursa ya kutafakari maisha ya Bwana Yesu katika kipindi hiki cha pasaka kutafuta na kupata mwafaka. Tunaweza”

Kutoka Facebook.