Zifuatazo ni kauli zilizotolewa na viongozi mbalimbali wa zile kamati
kwenye bunge la katiba linaloendelea pale Dodoma ambapo viongozi hawa leo April/14/2014 wameendelea kuwasilisha taarifa kutoka kwenye kamati zao..
Ni maoni ya pande mbili ambazo ni maoni ya wengi ambao ndio
wanaounga mkono serikali mbili alafu maoni ya wachache ambao wanaunga mkono
uwepo wa serikali tatu.
TUNDU LISSU: “Nusu
karne ya uongo iishe, Tanganyika iliuwawa na amri za Mwalimu Nyerere na hakuwa
na mamlaka kisheria kuiua, hatujawahi kuwa nchi moja, habari ya Tanzania kuwa
nchi moja iliingizwa ktk katiba miaka 20 baada ya muungano, nchi hii ni
haramu…. miaka 50 ya kudanganyana ikome, nchi hii inahitaji kuelezwa ukweli”
MCHUNGAJI MTIKILA: “tulijengwa kwenye misingi ya uongo ndio maana Mungu
alishindwa kubariki hii nchi yetu kwa miaka 50, uongo tuuondoe, swala la
muungano lilikua utapeli wa kisiasa, tuurudie ukweli kuhusu uhuru wa
Watanganyika na Wazanzibari”
MH WASSIRA: “Hati
ya Muungano ipo, naahidi
kwa niaba ya Jamuhuri itawasilishwa kwa Mwenyekiti ndani ya siku mbili zijazo, kama Wananchi wangetoa maoni kutaka kuvunja muungano, je tume ingeyaleta? serikali 3 italeta mgongano”
kwa niaba ya Jamuhuri itawasilishwa kwa Mwenyekiti ndani ya siku mbili zijazo, kama Wananchi wangetoa maoni kutaka kuvunja muungano, je tume ingeyaleta? serikali 3 italeta mgongano”
MH WASSIRA: “Katiba
ya Z'bar ndio itabakia kuwa sheria kuu kwa Z'bar kwa mambo yasiyokua ya muungano,
tukiweka serikali 3 hapa zikaweka masharti kuna watu watapata matatizo, itapunguzia
Wazanzibari fursa”
ISMAIL JUSSA: “Hoja
za historia kwamba tulikua vipi haziwezi kulibakisha taifa katika mgando,
ukiangalia katiba ya muda ya mwaka 1965 inaendelea kuitambua Tanganyika na
kuwepo makamu wawili wa Rais”
ISMAIL JUSSA: “Mkataba
wa muungano haukutoa mamlaka kwa chombo chochote kubadilisha kilichopo ndani,
ajabu bunge limefanya, tunapokua Znz tunasema mengine tukija huku tunaufyata,
Wazanzibari watatuhukumu”
ISMAIL JUSSA: “Z'bar tumeachwa watupu, tumechoka na hatukubali tena,
ktk mfumo wa serikali mbili Z'bar haitaweza kujisimamia kamwe, hatutakubali
kuendelea nao”
ISMAIL JUSSA: “Kama
kuna nia njema kwa nini kuna kufichaficha, mfano mwingine hai ni Rais wa Z’bar kuondolewa
kuwa makamu wa Rais”
Chanzo MILLARDAYO.COM na TBCtv