Mfululizo wa aya 13 za Mambo muhimu aliyoyazungumza njumbe wa bunge maalum la katiba Profesa Ibrahim Haruna Lipumba akichangia mjadala wa jumla wa sura ya 1 na ya 6 ya rasimu ya katiba jana dakika 11 kabla za kuwaongoza wajumbe wa bunge hilo wa kutoka upande wa upinzani maarufu kama UKAWA kutoka nje ya bunge kwa HASIRA.
“Mimi
ni muumini wa dini ya mwenyezi Mungu, lakini naafiki mapendekezo yaliyoletwa
kwetu na tume ya jaji Warioba ambayo ni tume iliyoundwa na rais”.
“Gazeti
la Mwananchi la tarehe 14/Aprili/2014, limeandika kuwa.. nanukuu “Waziri wa nchi
ofisi ya Waziri mkuu sera, uratibu na bungeni mh. William Lukuvi ameanza
kampeni kanisani, kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na
tume ya mabadiliko ya katiba vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa
serikali ya muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi”. Hii ni kauli ya
waziri Lukuvi ndani ya kanisa la Methodist wakati wa sherehe ya kumsimika
mchungaji Joseph Bundala kuwa Askofu na waziri Lukuvi alikuwa anamuwakilisha
waziri mkuu.”
“Zitto
Kabwe asubuhi ya leo, ameeleza vizuri kwamba tatizo letu ni usmamizi mzuri wa
mapato yetu ya nchi kwamba muungano kuvunjika hauvunjiki kwa sababu ya serikali
1, 2 au 3, ni utashi wa kisiasa na haya ni maneno pia, vice chancellor wangu
Pius Msekwa alishayazungumza.”
“Kama
ndugu zetu waz’bar, wangekuwa wanahitaji
muungano wa serikali moja, tungekuwa,
na utaratibu mzuri tu wa serikali moja. Lakini siyo wanachama wa CUF,siyo
wanachama wa CCM, waz’bar hawataki muungano wa serikali moja. Tume ya jaji
Warioba kutoa mapendekezo ya serikali 3 ni kutokana na ukweli huo, hoja
zinazoletwa hapa ni hoja za serikali 1 siyo hoja za serikali 2, lakini wenzetu
serikali 1 hawataki. Kwa hiyo tunahitaji kuwa na muungano amabo tutakuwa na
maridhiano ya pande zote mbili”.
“Wengi
wamenukuu makala niliyoitoa katika kikao cha TCD, TCD iliunda baraza la katiba,
na mimi nilichambua mapendekezo ya tume, nikasema kwa mapendekezo yaliyomo
ndani ya rasimu ya katiba hayatakidhi mapato ya serikali ya shirikisho. LAKINI
WANAONINUKUU WANAISHIA HAPO HAWAENDI KWENYE MAPENDEKEZO NILIYOTOA. Wamenisifu
saana ni mchumi mahiri basi waendeleze sifa hizo kwa mapendekezo niliyoyatoa ya
KUKIDHI MAHITAJI YA MAPATO YA SERIKALI YA SHIRIKISHO. Na nimeeleza, kwamba
katika hali halisi, UTARATIBU MZURI NI MAPATO YA KILA SERIKALI KUCHANGIA MAPATO
YA SHIRIKISHO na mambo haya yaandikwe ndani ya katiba. Katiba inaweza ikasema
wazi 20% ya mapato yote yanayokusanywa Z’bar na yanayokusanywa Tanzania au
Tanganyika yataenda kwenye serikali ya shirikisho. Na tuweke misingi mizuri ya kukusanya
kodi na ya kutumia fedha za wananchi ndani ya katiba ya muungano ambayo ndiyo
katiba mama. Na mambo haya yanawezekana.”
“Lakini
ndugu zangu mjadala wetu unavyokwenda, utadhani rasimu iliyoletwa na serikali, imeletwa ama na CUF au na
CHADEMA au NCCR au Wapemba!”
“Ukurasa
wa kwanza wa rasimu unaeleza kwamba
toleo hili la rasimu ya katiba linachapishwa kwenye gazeti la serikali
kwa mujibu wa kifungu cha 20 (2) ya sharia ya mabadiliko ya katiba sura ya 83
na itawasilishwa kwenye bunge maalum la katiba kwa ajili ya kujadiliwa na
kupitishwa na Jakaya Mrisho Kikwete rais. HII NI RASIMU YA TUME YA RAIS, siyo
rasimu ya wapemba”.
“Lakini
katika mjadala wetu hapa, Mjadala umekuwa na utaratibu wa ubaguzi!, watu
wamebaguliwa humu, na VIONGOZI WAKUBWA WANAPIGA MAKOFI! Bunge hili limekuwa
kama bunge la INTARAHAMWE! Hii ni HATARI kwa nchi yetu! Wapemba., Waarabu..,
Wahindi.., Wakongo.., Wahadimu hii hatuhitaji ubaguzi katika nchi hii”.
“Tunahitaji
katiba ambayo itahakikisha kila mwananchi anapata haki yake, wote tuwe sawa
bila kujali rangi zetu, jinsia zetu, makabila yetu huu ndiyo msingi aliotuachia
mwalimu Nyerere, tuuenzi msingi huo. Tusiweze kunza kufanya ubaguzi na ubaguzi
umefanyaka ndani ya bunge hili”.
“Na
kauli za waziri zinatisha zaidi, anapoeleza ndani ya kanisa kwamba waz’azr
wanaotaka kuwa nan chi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka serikali ili
wapate nafasi ya kujitangazia kuwa ni nchi ya Kiislamu. Waziri anaenda kusema
hivyo ndani ya kanisa! Kawahamasisha mpaka yule kiongozi wa kanisa akaeleza
kwamba, Askofu Bundala alisema kanisani hapo kwamba ili kudumisha muungano ni
vyema katiba ya Z’bar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha
muungano, Mwisho wa kunukuu. Waziri wa nchi! na anakwenda kule kumwakilisha
waziri mkuu, anatamka maneno kama haya!”.
“Sasa
kama mlikuwa mnajua kwamba rasimu ya katiba ikipitishwa patakuwa na mapinduzi
katika nchi, nchi haitatawalika, watu hawataweza kwenda kusali makanisani KWA
NINI MLITULETA HAPA?, kwa nini mmetumia BILLION
60, BILLION 70, Kwenye tume ya Jaji Warioba?, Kwa nini mmetufikisha hapa?
“Jengo
hili naambiwa limekarabatiwa kwa shilingi BILLION 8.2, hali hamuiamini rasimu
ya katiba! Ama ilikuwa utaratibu wa kupata hizo ‘Ten Percent’ ndiyo maana
mmeratibu mmekarabati kwa gharama kubwa? Tunawataka.. CAG akague! Akague
matumizi ya fedha zilizofanyika, Utatumiaje fedha nyingi wakati hiyo katiba
inayowakilishwa kumbe hauitaki kabisa?”
“Tumechoka
kusikiliza matusi! TUMECHOKA kudharau mawazo ya wananchi, TUMECHOKA ubaguzi.
Hatuwezi kuwa sehaemu ya kundi la INTARAHAMWE linalohamaiisha ubaguzi ndani ya
Tanzania, hili hatulikubali, hatulikubali, hatulikubali, watu wote tunaotaka
katiba ya wananchi tunawaachia muendelee na kikao chenu.Ahsanteni sana".
Mara baada ya kusema
hivyo, wajumbe waliounga mkono kauli yake waliinuka na kutoka nje.
Hata hivyo, kikao cha
bunge hilo kiliendelea baada ya makamu mwenyekiti wa bunge hilo kusema idadi ya
wajumbe waliobaki walitosha kuendelea na kikao hicho.
Wanaounga mkono muundo
wa serikali tatu, wanasema muundo wa sasa wa serikali mbili umeshindwa kutatua
masuala yenye mgogoro katika muungano, maarufu kama kero za muungano, hivyo
kudhoofisha muungano huo.
Hata hivyo wajumbe
wanaounga mkono serikali mbili, yaani serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wanasema muundo wa serikali tatu ni
kuvunja muungano wa Tanganyika na Zanzibar na pia itakuwa gharama kuiendesha
serikali ya tatu.
Bunge hilo lenye zaidi
ya wajumbe 600 linaundwa na wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Baraza la wawakilishi Zanzibar na wajumbe 201 walioteuliwa na rais wa
Tanzania kutoka makundi mbalimbali ya kijamii.
Wajumbe 191 kutoka upinzani
walitoka nje ya bunge kupinga mwenendo wa bunge hilo katika kujadili rasimu ya
katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
UNAWEZA SIKILIZA MCHANGO WA PROFESA IBRAHIM LIPUMBA HAPA CHINI