Meneja David Moyes amepigwa kalamu na Manchester
United, klabu hicho kimetangaza Jumanne baada ya msimu wake wa kwanza kugeuka
kuwa janga kubwa kwa magwiji hao wa Uingereza.
“Manchester
United wanatangaza kuwa David Moyes ameondoka kwenye klabu hiki,” United
walichapisha kwa anwani yao rasmi katika mtandao wa kijamii wa Twitter.
“Klabu
hiki kingependa kumshukuru kwa bidii, uadilifu na unyofu alioleta kwa wadhifa
wake.”
Habari
za kutimuliwa kwa Moyes zilijili baada ya vyombo vya habari Uingereza kutangaza
kuwa utawala wa miezi 10 wa Moyes unayoyoma baada ya kumrithi gwji Sir Alex
Ferguson aliyestaafu msimu jana.
Raia
huyo wa Scotland 50, amejipata kwa balaa moja hadi nyingine huku United,
mabingwa wa ligi ya Premier wakishuka hadi nafasi ya saba na kuchakazwa kao 2-0
na Everton Jumapili kulidhibitisha hawatafuzu kombe la mabingwa kwa mara ya
kwanza tangu 1995.
United
wamo alama 13
nyuma ya nafasi ya nne na 23 nyuma ya watanashari wao Liverpool wanaopigiwa upatu kuwaridhi kama mabingwa wa Premier ikisalia mechi nne muhula huu kwisha.
nyuma ya nafasi ya nne na 23 nyuma ya watanashari wao Liverpool wanaopigiwa upatu kuwaridhi kama mabingwa wa Premier ikisalia mechi nne muhula huu kwisha.
Kulingana
na duru, afisa mkuu mtendaji wa United, Ed Woodward, aliarifu Moyes binafsi
uamuzi wa kumpiga kalamu katika makao yao ya Carrington Jumanne asubuhi.
Mkongwe
Ryan Giggs na mwenzake Nicky Butt wanatarajiwa kuchukua hatamu za uongozi kwa
muda na kuongoza United dhidi ya Norwich City Jumamosi huku miamba hao wakisaka
mrithi ambaye atarejesha hadhi yao.
Louis
van Gaal, kocha wa Uholanzi, amepigiwa upatu na wadau kuchukua wadhifa huo huku
Jurgen Klopp (Borrusia Dortmund), Diego Simeone (Atletico Madrid) na Giggs
wakitajwa kama wengine wanaowazwa na bodi ya klabu hicho.
kutoka Supersport.com