Saturday, April 26, 2014

Tsvangirai asimamishwa uongozi MDC

Chama cha upinzani nchini Zimbabwe cha Movement for Democratic Change MDC kimemsimamisha kiongozi wake Morgan Tsvangirai kwa kukiuka kanuni za kidemokrasia.

Katibu Mkuu wa MDC Tendai Biti, amethibitisha hilo katika mkutano wa chama hicho uliofanyika katika mji Mkuu Harare.

Tsvangirai alitumikia taifa la Zimbabwe katika nafasi ya
Waziri Mkuu katika serikali ya umoja wa kitaifa iliyoundwa kwa pamoja na Rais wa sasa Robert Mugabe tangu mwaka 2009 hadi 2013.

Serikali ya Umoja wa Kitaifa ilifikia kikomo mwezi julai mwaka 2013 baada ya Rais Mugabe kushinda kwa wingi wa kura katika uchaguzi wa rais na Tsvangirai kususia uchaguzi kwa madai ya udanganyifu.

Kushindwa kwa Tsvangirai kulipunguza nguvu yake kama kiongozi ambaye alikuwa mshindani mkuu wa Rais Mugabe.

Waangalizi wanasema ndani ya MDC kumekuwa na mgogoro wa kiuongozi kwa miezi kadhaa.

Hata hivyo viongozi wengine wa ngazi za juu wameripotiwa kusimamishwa katika mkutano huo uliofanyika siku ya jumamosi na wanachama wengine wa chama hicho watachukua nafasi zao.

Na. Gwalugano Mwakalobo, kutoka bbc.com/swahili