Tuesday, March 11, 2014

SITTA KUMBADILI PANDU KIFICHO


Samwel Sitta akipokea fomu ya kugombea nafasi ya kuwa mwenyekiti wa bunge maalum la katiba kutoka kwa ofisa wa bunge bi Lidya Mwaipyana na katikati ni mbunge wa Nzega Dk. Hamisi Kigwangala mmoja wa wajumbe wa bunge maalum la katiba.



Aliyekuwa spika wa bunge la 9 la jamhuri ya muungano wa Tanzania mh. Samuel Sitta amechukua fomu ya kuwania nafasi ya kuwa mwenye kiti wa bunge maalum la katiba.

Katika hilo mh. Sitta  ametoa ahadi ya kusimamia haki kwa makundi yote likiwemo kundi la wajumbe mia mbili na mmoja (201) lililoteuliwa na Mheshimiwa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania  Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.